.........BLOG HII BADO IPO KWENYE MATENGENEZO......

Jumanne, 24 Aprili 2012

Mhe. Mkono alamba sahihi kwenye karatasi ya Zitto




Juzi usiku Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec) na Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, juzi usiku alisaini fomu ya majina ya wabunge wasiokuwa na imani na Waziri Mkuu yanayokusanywa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto kabwe.

Zitto alikuwa akikusanya saini za wabunge wasiopungua 70 ambao ni asilimia 20 ya wabunge wote ili awasilishe hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu kwa Spika wa Bunge.

Mkono alikuwa ni mbunge wa 74 na wa sita wa CCM kati ya 76 waliosaini fomu hiyo hadi jana mchana. Juzi usiku, Mkono alimpigia simu Zitto na kumtaka ampelekee fomu hiyo ili aweke saini yake.

“Mimi ni mjumbe wa NEC na nimepata nafasi hiyo kwa kuchaguliwa na wabunge wenzangu wa CCM, sasa ninapoona wabunge wenzangu wakiwemo wa CCM wanalalamikia utendaji wa mawaziri wetu kwa kuhusishwa na ufisadi wa fedha za umma na Serikali inakaa kimya ni lazima nichukue hatua,” alisema na kuongeza:

“Mawaziri wetu hata wafanye kosa gani sisi wabunge hatuwezi kuwawajibisha, ni mmoja tu naye ni Waziri Mkuu ambaye tunaweza kufanya hivyo. Sasa tumeona kuna mawaziri wamekutwa na kashfa mbalimbali na bado wanang’ang’ani kubaki kwenye nafasi zao hatuna jinsi, ili kuwang’oa nilazima tumuondoe Waziri Mkuu.”

“Sina tatizo na Pinda katika utendaji wake wa kazi lakini hatuwezi kuwaondoa mawaziri wenye kasoro bila ya kumwondoa yeye kwa mujibu wa sheria zetu, ndiyo maana nimesaini fomu hii kwa maslahi ya taifa langu.”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni